![Ripoti za Mtaani ft. Zahir Zorro](https://source.boomplaymusic.com/group2/M09/CE/90/rBEeM10oONuAXC2OAADZ_fXsM2w734.jpg)
Ripoti za Mtaani ft. Zahir Zorro Lyrics
- Genre:Hip Hop & Rap
- Year of Release:2009
Lyrics
Ripoti za Mtaani ft. Zahir Zorro - Fid Q
...
inasikitisha ina huzunisha inasikitisha!!
maisha ni safari ambayo tayari imekwisha kwa zake juhudi
alipokimbilia ni mbali michosho akifikiria kurudi
pole pole ndo mwendo kila akikumbuka ina muuma kwanza viliumbwa vidole binadamu ndo akaumba uma anaamini ye nimwema na wabaya mungu hawahitaji samaki anamengi ya kusema lakini mdomoni anamaji muadithiaji akiwa mmoja story huaga haikamiliki msishereheshe bora mjivishe viatu vya huyu binti aliye mtunza miezi9 tumboni ndiye aliye mfunza kutambaa kabla hajaanza kutembea lakini babaake aliye mzaa alimshauri aache shure ili aolewe kwa sababu mama hanasauti aliona bora tu amuelewe
bora aolewe tu na huyu kijana japo hajamrithia moyoni kwakua mwanzo ashaujua haiwezi kumsumbua mwishoni kadri unavyo mzengua paka huzidi nyanyua mkia ghafla akaitamani talaka akageuka kiruka njia mwana akagida sumu akafa alidata baada ya kusikia dem ashamkomba mikwanja amesonga kiwanja amemkimbia anachukuliwa tu na wajanja hajui kubana ye huachia binti hakuacha mlango wazi ili wageni wasigonge sana
hakujua haya mambo yanaweza kumuharibia usichana akaonekana hana mpango mrembo kwa starehe za ujana tangu hofu yake sio mdebwedo anakimbiwa tu na hao mabwana wakwanza alimpata club binti akafika kikweli akamvisha mng'alo wa silva mkubwa zaidi zaidi ya wynnwell sikuzikapita kimaisha akaanza kufeli kwakua uongo alizidisha amejikuta yuko nje ya ukweli!!
(chorus)
mmmh iiiiiiiiiii
inasikitisha ina huzunisha
(inaniuma sana)
inasikitisha kama kokote imekwama na
lazima niseme aaah na lazima nisemee
uuuuuuuuuuuh
nahizo ndizo ripoti za mtaani
nahizo ndizo ripoti za mtaani
lazima niseme
alipenda kwenda na tarehe akasahau siku hazilingani pesa huja na starehe na matatizo humohumo ndani hakuna kinacho kauka mapema zaidi ya machozi japo macho hubaki mekundu na usoni ishara ya majonzi kizuri ni kizuri lakini chenye ubora ni bora kwa bahati nzuri au mbaya akaja mchimba madini wa kakola akashoboka na huyu binti wa mjini aliye msafisha macho
aka muhonga gari nyumba na kila alicho kuwa nacho amesahau alitoa machozi damu na jasho kipindi ana hustle siku si nyingi anaamini atarudi hapohapo!!
siku zote Adam hakosi Eva wa kumshawishi haijalisi maji ni yamoto lazima ataurudia ubaridi akipumzisha utaota kutu wakati kitu sio funguo namuomba mungu amsitili zaidi ya mwili Wake na nguo hakutaka kuonekana kama kifaranga cha kuku kila siku atanyonya kesho wakati maziwa iko huku kijana akawa mchezaji zaidi ya Ronald wa Brazil tisa ukiongeza moja bado haikamilishi dozen usiombe alio wavisha kofia wote hawakua na vichwa alicho poteza akihesabu alicho bakiza
inasikitisha ina huzunisha
inaniuma sana
kama popo nimekwama
ooooh lazima niseme
lazima niseeeme
lazima
lazima niseme
lazima
ndiyo
lazima niseme