UMBEA Lyrics
- Genre:Gospel
- Year of Release:2024
Lyrics
Umbea umbea kati ya wakristo
Umetoka wapi twahubiri nini
Umbea manyumbani umbea kanisani
Fitina masengenyo acheni kabisa
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa
Kanisani leo hata nashangaa
Mbona watu waenda kuzusha umbea
Atasimama mbele yenu dada aliyevaa nadhifu
Awatolee ushuhuda kumbe ni mzushi
'Kimshinda kwa mavazi aanza uzushi
Akusingizia asema wewe msherati
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa
Hamtaki nivae wala 'niendelee
Mradi naongoza mwaanza maneno
Nikijenga nyumba ninunue gari
Mwaanza kusema nala pesa za kanisa
Wewe hutoa ngapi kati ya sadaka
Ama zako zaliwa zingali mfukoni
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa
Nikibarikiwa na pesa na mali
Nawe ni mkristo waanza kuzusha
Ashasoma dini ya shetani amwabudu ibilisi
Mwaniharibia sifa Mungu 'tanilipia
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa
Mwana mume na mke wakisikizana
Waanza uzushi mume kapewa madawa
Hawa wapendana tena ndoa yao
Wanaidhamini sana mambo hutenda kwa ushirika
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa
Umbea umbea umbea umbea
Kati ya wakristo acheni umbea
Shughulikieni yenu acheni uzushi
Mambo yasiyofaa acheni kabisa